Friday, 2 September 2016

Wanajimu katika maeneo tofauti ya bara Afrika wameona moto wa mviringo angani wakati wa kupatwa kwa jua.

Jua hupatwa wakati ambapo mwezi huwa mbali na dunia ikilinganishwa na wakati jua linapopatwa kabisa.
Matokeo yake huwa ni mviringo mkubwa unaong'aa ukiwa umezunguka eneo jeusi .
Picha nzuri ni zile zilizoonekana nchini Tanzania ambapo tukio hilo lilichukua mda wa dakika tatu.
Kupatwa huko kwa jua pia kulionekana nchini Gabon,Congo-Brazaville,DRC Madagascar na kisiwa cha Re-union.
Wakati ambapo mwezi uko mbali na dunia ,huonekana mdogo na hauwezi kuliziba jua kabisa wakati wa kupatwa kwa jua.Matokeo yake hujulikana kama mviringo wa moto.
Kupatwa kwengine kwa jua kunatarajiwa kufanyika mnamo mwezi Februari 2017 na huenda kukaonekana katika maeneo ya Marekani kusini na Africa.

Mwanzilishi wa kampuni ya facebook Mark Zuckerberg amezuru nchini Kenya katika ziara yake ya mataifa ya bara Afrika.

Zuckerberg aliyewasili siku ya Jumatano kutoka nchini Nigeria alifanya kikao na waziri wa habari nchini Kenya Joseph Mucheru,ambapo walizungumza kuhusu mtandao na mipango ya serikali kuhakikisha kila kijiji kimeunganishwa na mtandao.
Baadaye Zuckerbag aliekea katika hoteli ya Mama Oliech katika chakula cha mchana ambapo kwa mara ya kwanza alikula Ugali na Samaki.
''Swala muhimu ninapozuru taifa lolote jipya ni kujaribu kula chakula chao.Nilipenda sana ugali na samaki mzima wa tilapia'',alisema Zuckerberg.

Wednesday, 17 August 2016

Rais wa zamani wa FIFA Joao Havelange afariki dunia

Rais wa zamani wa FIFA Joao Havelange amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 100.Mbrazil huyo alikuwa mtangulizi wa Sepp Blatter katika shirikisho la mpira wa miguu duniani kuanzia mwaka 1974 hadi 1998.
Alijiuzulu nafasi ya Urais wa FIFA April 2013 kufuatia uchunguzi wa madai ya kupokea rushwa,na kulazwa
hospitalini mwaka uliofuata alipokumbwa na ugonjwa wa mapafu.
Alikuwa mmoja wa wanakamati wa Olympic (IOC), kuanzia mwaka 1963 hadi 2011 alipojiuzulu kwa sababu ya kudhoofu kwa afya yake.
Havelange aliiwakilisha Brazil katika mashindano ya Olympic ya Kuogelea mwaka 1936,mwaka ambao aliidhinishwa kuwa mwanasheria kabla ya kuchaguliwa na IOC.
Akiwa kiongozi wa FIFA aliongeza washiriki wa kombe la dunia kutoka timu 16 hadi 32, ambapo mashindano 6 yalifanyika chini ya utawala wake.

Tuesday, 16 August 2016

Conte awa kuvutio

Kocha wa Chelsea Antonio Conte awa kivutio katika game ya kwanza ya Premier league .
Chelsea ilifanikiwa kuwafunga wangonga nyundo wa London kwa goli 2 kwa 1.
Hazard kwa penalty na Costa dk.89.
Hivyo na kufanya makocha wapya wote kuanza  kwa ushindi.

Rio 2016: Usain ashinda dhahabu ya mita mia 100 akifuatwa na Justin Gatlin

Mwanariadha wa Jamaica, Usain Bolt, ameandikisha historia ya kuwa mwanariadha wa kwanza kushinda nishani ya dhahabu kwa mara ya tatu mfululizo, katika mbio za mita mia moja, kwenye michezo ya olimpiki ya Rio 2016.
Bolt, 29, amechukua muda wa sekunde 9.81 katika fainali yake ya mwisho katika michezo ya olimpiki, kwa kuiga ushindi sawa na huo katika michezo ya olimpiki mjini Beijing 2008, na London 2012.
Gatlin, ambaye amepigwa marufuku mara mbili kwa matumizi ya dawa za kutitimua misuli, alimaliza sekunde 0.08 nyumna ya Bolt na kuchukua nishani ya fedha.
"Nilitarajia kwenda kasi zaidi, lakini nafurahia kwamba nimeshinda," Bolt ameiambia BBC.
Mwanariadha wa Canada Andre de Grasse ameshinda nishani ya shaba, na kuandikisha muda bora wa kibinafsi wa sekunde 9.91, mbele ya mwanariadha wa Jamaica Yohan Blake.
Bolt anatazamia kuondoka Rio na nishani zaidi za dhahabu katika mbio za mita 200 na mita 100 kupokezana vijiti, jinsi ilivyokuwa katika michezo ya olimpiki ya mwaka 2008 na 2012.
Mwanariadha huyo anayeshikilia rekodi ya dunia katika mbio za mita 100 alisema kuwa atastaafu kutoka kwenye ulingo wa riadha baada ya michuano ya ubingwa dunia mwaka 2017.

Homa ya manjano ni tishio ulimwenguni

Shirika la kimataifa la Save the Children limetahadharisha kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa homa ya manjano katika nchi za Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Angola kuwa hivi karibuni unaweza kuenea katika nchi za mabara ya ulaya , Amerika na Asia.
Ugonjwa huo unaenezwa na mbu aina ya aedes, wanaopatikana katika nchi nyingi za Afrika Magharibi.
Mlipuko wa ugonjwa huo barani unaelezwa kuwa mkubwa kuliko miaka 30 iliyopita na umesababisha kutumika kwa chanjo mara nne kuliko ilivyo kawaida kwa mwaka huu pekee jambo lililofanya Shrika la Afya duniani WHO kupunguza kiwango cha dozi ili kuwezesha watu wengi zaidi kupata chanjo hiyo.
Shirika hilo la Save the children limesema limetuma wataalamu wake kusaidiana na serikali ya DRC kutoa chanjo homa hiyo ya manjano kwa watu nusu milioni katika mji mkuu wa Kinshasa.
Tayari mzungumko wa kwanza wa chanjo hiyo ilishatolewa katika mji huo wa Kinshasa baada ya kuthibitishwa kulipuka kwa ugonjwa huo ambao hauna tiba.
Awali ugonjwa huo uliripotiwa katika nchi jirani ya Angola kabla ya kuenea nchi Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Zaidi ya watu mia nne walioambukizwa ugonjwa huo wamefariki katika nchi hizo mbili ambapo huku wengine zaidi ya watu elfu sita wakiripotiwa kuambukiza ugonjwa huo.
Shirika la afya ulimwenguni WHO limesema hakuna maambukizi mapya yaliyoripotiwa nchini Angola tangu mwezi juni , na kufufua matumaini kwamba ugonjwa huo sasa utadhibitiwa.

Mtoto Zephany Nurse aibwa hospitali Afrika Kusini

Mahakama moja nchini Afrika Kusini imemhukumu mwanamke mmoja kifungo cha miaka kumi jela kwa kosa la kumteka nyara mtoto mchanga yapata miaka ishirini iliyopita na kumkuza huku akimuamisha kuwa yeye ndiye mama yake mzazi.
Mwanamke huyo sasa ana umri wa miaka hamsini amekana madai ya yanayomkabili ya udanganyifu na utekaji nyara.Muuguzi Zephany anasema mtoto huyo mchanga alinyakuliwa alipokuwa amelala kwenye kitanda kando y mama yake katika hospitali iliyoko mjini Cape Town.
Tuhuma dhidi ya mwanamke huyo zilianza tangu mnamo mwaka jana mara baada ya binti aliye mwiba kuanzisha urafiki baina yake na msichana mdogo aliyekuwa anasoma naye kufanana mpaka kutia fora.Uchunguzi wa vinasaba ulipofanywa, watoto hao waligundulika kuwa ni ndugu.
Hakimu Hlope alimwambia mshtakiwa kwamba ameidanganya mahakama yake na haonekani kujutia kosa lake.

Aboud Jumbe aaga dunia kigamboni jijini

Rais mstaafu wa awamu ya pili ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mzee Aboud Jumbe Mwinyi amefariki dunia Jumapili saa saba mchana nyumbani kwake katika kijiji cha Mji Mwema, eneo la kigamboni jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Bwana Mohamed Aboud, mwili wa Mzee Aboud Jumbe Mwinyi ambaye pia alikuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unatarajiwa kusafirishwa Jumatatu kwa ndege kuelekea visiwani Zanzibar kwa ajili ya maziko.
Bwana Mohamed Aboud amesema Marehemu Aboud Jumbe Mwinyi anatarajiwa kuzikwa nyumbani kwake eneo la Migombani, Mkoa wa Mjini Maghrib mnamo saa saba za mchana. Marehemu amefariki akiwa na umri wa miaka 96 alizaliwa June 14, 1920 huko Juba, Sudan Kusini.
Aidha viongozi mbalimbali wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wanatarajia kuhudhuria maziko hayo ya Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi .
Marehemu Aboud Jumbe Mwinyi alishika wadhifa wa Rais wa Zanzibar April 7, 1972 mara tu baada ya kifo cha aliyekuwa rais wa kwanza wa visiwa hivyo Abeid Amani Karume. Hayati Aboud Jumbe alijiuzulu urais wa Zanzibar pamoja na nyadhifa nyingine za makamu mwenyekiti wa CCM na makamu rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Januari 30, 1984.
Mungu alizale roho ya Marehemu mahali pema peponi

Monday, 8 August 2016

"NINA UHAKIKA NA UBINGWA MSIMU UJAO"- GEOFREY NYANGE 'KABURU'

Makamu mwenyekiti wa klabu ya Simba, amewaambia mashabiki wa timu hiyo kujiandaa na Ubingwa wa ligi ya Vodacom msimu ujao.
Kaburu ameiambia Goal kwamba mabadiliko ya kikosi walichosajili kwa ajili ya msimu ujao ndivyo vinavyo wapa matumaini ya kubeba taji hilo msimu ujao.
"Mabadiliko yetu hayapo kwenye uongozi bali hata usajili wetu wa msimu ujao umetulia tumesajili vizuri na ninauhakika na ubingwa msimu ujao" amesema kaburu.
Simba ambayo msimu ujao itakuwa chini ya kocha Mcameroon Joseph Omog jana ilikamilisha usajili wake wa msimu ujao akiwemo mchezaji Lodit Mavugo aliyetokea Vital'o ya Burundi.

JOSE MOURINHO: "HATIMAYE TUMEMPATA PAUL POGBA"

Meneja wa Manchester United, Jose Mourinho amekiri kuwa "hatimaye" klabu yake imefanikiwa kuipata huduma ya Paul Pogba kutoka Juventus
Mustakabali wa Pogba ulikuwa umezungukwa na tetesi nyingi mno majuma ya hivi karibuni, kwa nyota huyo kusajiliwa kwa ada ya kuvunja rekodi na Mashetani Wekundu.
Uthibitisho rasmi ulipatikana leo kutoka klabuni hapo kwamba Mfaransa huyo amepewa ruhusa na Juventus kuendelea na vipimo Manchester, lakini Mourinho ameonya kuwa hana uhakika wa namba katika kikosi chake.
"Pogba? Hatimaye, ni mchezaji mahiri. Mchezaji mzuri kama yeye atakuwa pamoja nasi, hatimaye tunaye," alisema Mourinho.
"Hatimaye tunaye. Anaungana na kikosi cha ushindi. Lakini atalazimika kufanya bidii nyingi kuingia kwenye kikosi. United ni klabu sahihi ambayo itamweka kwenye viwango anavyohitaji kuwa.
"Nimemwona Pogba akikimbia, akicheza kikapu, hufanya kila kitu, kwahiyo natumai atakuwa fiti. Nitakuwa nikimsubiri Jumanne."
Mourinho amenyanyua taji lake la kwanza kama meneja wa United kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Leicester City katika mechi ya Ngao ya Jamii iliyopigwa Wembley Jumapili mchana.

Oscar Pistorius ajeruhiwa gerezani

Msemaji wa idara ya magereza nchini humo, amesema kuwa Pistorius alianguka kutoka juu ya kitanda chake, lakini kwa sasa amerejeshwa gerezani anakohudumia kifungo cha miaka sita kwa kosa la kumuuwa mpenziwe wa kike Reeva Steenkamp.
Kuna ripoti inayosema kuwa alikuwa amejeruhiwa kwenye kifundo cha mkono.
Kumeibuku uvumi katika mitandao ya kijamii nchini Afrika Kusini kuwa Pistorius alikuwa amejaribu kujitia kitanzi lakini hilo limekanushwa na familia ya mwanariadha huyo.
Mwezi uliopita, waendesha mashtaka nchini Afrika Kusini, walisema kuwa watakata rufaa kupinga hukumu ya miaka sita ya Pistorius, wakisema kuwa ni hukumu ndogo mno.
Mwanariadha huyo alimuuwa mpenziwe wa kike , kwa kumpiga risasi nyumbani kwake wakati wa siku kuu ya wapendanao mnamo mwaka wa 2013, akisema kuwa alidhania ni mwizi.

Sakata la Yanga

Nafurahi kuona Tanzania inafufuka katika sokaa!!
Natamani kuona kila pedeshyeeee akimiliki timu moja ya ligi juu na kujenga kiwanja maendeleo ya timu yasonge mbele!!!
Yanga na sakata lao muwaaachie wenyewe ,majibu mtayapata baaada ya miaka 4 ,natumai wengine mtajifunza hapo

Pogback

Pogba ameshatua London na ameshafanyiwa vipimo Leo kutangazwa rasmiii!!

Saturday, 30 July 2016

Wauawa kwa kushindwa kulipa deni la biskuti India

Mtu mmoja na mkewe kutoka jamii ya Daliti inayobaguliwa tangu jadi nchini India wameuawa, mmoja akiwa amekatwa kichwa na mwengine kunyongwa kwa kushindwa kulipa deni la Rupee kumi na tano ambalo ni karibu senti ishirini na mbili tu.
Polisi kaskazini mwa taifa hilo wamethibitisha kisa hicho ambapo yasemekana mfanyi biashara anayetokea jamii ya hadhi ya juu,aliwaua wanandoa hao kwa kushindwa kulipa deni la biskuti walizokuwa wamewachukulia watoto wao.
Mfanyi biashara huyo amekamatwa.
Ubaguzi kwa misingi ya kijamii umeenea sana nchini India, huku watu wa jamii ya Daliti waliokuwa wamebadikwa jina la 'the untouchables' wakiwekwa kwenye daraja la chini kabisa kwenye sera hiyo ya kibaguzi nchini India iitwayo 'caste' ambapo wananyimwa fursa nyingi za kimaendeleo na hivyo kubaki katika lindi la umaskini .
Hata hivyo Visa vya ukatili wa kibaguzi dhidi ya jamii ya Dalit katika jimbo la Gujarat vimeongezeka mnamo siku za hivi karibuni na vimesababisha wimbi la maandamano kutoka watu wa jamii hiyo.

Thursday, 28 July 2016

Chelsea 1 Liverpool 0: Cahill´s header seals win

Gary Cahill's first-half header was enough for a 10-man Chelsea to see off Liverpool 1-0 in their International Champions Cup fixture.
Defender Cahill rose highest from a Cesc Fabregas corner in the 10th minute, heading it past Liverpool goalkeeper Loris Karius for the only goal of the game on Wednesday.
Jurgen Klopp's side could not find a way past Asmir Begovic despite Fabregas being sent off for a crunching tackle on Ragnar Klavan in the 70th minute at the Rose Bowl in Pasadena, California.
The loss was Liverpool's first of the pre-season under Klopp, having secured victories over Tranmere Rovers, Fleetwood Town, Wigan Athletic and Huddersfield Town.
Here's @GaryJCahill celebrating his goal earlier on... #CFCTour pic.twitter.com/daAhxVsMhu
— Chelsea FC (@ChelseaFC) July 28, 2016
Youngster Ovie Ejaria looked bright for the Reds, but it was Chelsea who were carving the better of the chances throughout the opening period, with Fabregas and Victor Moses particularly threatening.
Liverpool recruit Marko Grujic was in the wars in the first period and had to be treated on the stroke of half-time after a clash of heads, and was replaced at the break by Adam Lallana.
Chelsea sat back in the second half as head coach Antonio Conte tinkered with his side, with Juan Cuadrado, Pedro and new signing Michy Batshuayi entering the fray.
However, just three minutes later Conte's side were dealt a blow after Fabregas was given his marching orders for a studs-up challenge on Estonian defender Klavan.

Klopp reveals why he sent Sakho back to Liverpool

Jurgen Klopp has revealed his fury with Mamadou Sakho after he sent the French defender home early from Liverpool's tour of the United States.
The German revealed that Sakho - who has only recently been cleared of a doping violation which he served a provisional suspension for - had broken team rules three times and now faces crunch talks to save his Liverpool career.
"He nearly missed the departure of Liverpool [on the plane from Liverpool to San Francisco], he missed a training session and was late for a team meal," said Klopp.
"I have to build a group here and we’ve got to start new here. I thought it maybe made sense for him to fly home to Liverpool.
"We have some rules and we have to respect them – if somebody gives me the feeling they are not respecting it I have to react.
"After eight or ten days we can talk about it. We had no argument but I spoke - you cannot argue when only one person is speaking."
When asked if Sakho would be fined, Klopp said he preferred alternative methods of punishment as he seeks a considered and calm outcome to the dispute.
"Fine him? You can ask, and I can explain it in general. I am not interested in the money of the players, actually not really often in my life I have had to fine anybody because I want that we learn together to do the thing that is right.
"Always it is the same with every group. I don't like fining. Sometimes it's funny, when the fine is bulls***. Come on, pay for it, that's nice. But mistakes, fining never helps.
"It's not because they care about money, it's always 'yeah in the moment it hurts but after a while not'. So I want them to do the things because they want to do it, that's

Yanga yazidi kuwa na matumaini

Wednesday, 18 May 2016

Aveva: Wachezaji wasio waaminifu wameiangusha Simba

Rais wa Klabu ya Simba Evans Aveva



Evans Aveva ametaja sababu kadhaa za timu hiyo kufanya vibaya msimu huu, mojawapo ni kuwa na wachezaji wasio waaminifu baadhi yao beki Hassan Kessy na mshambuliaji Ibrahim Ajib
Rais wa Simba SC, Evans Aveva ametaja sababu kadhaa za timu hiyo kufanya vibaya msimu huu, mojawapo ni kuwa na wachezaji wasio waaminifu baadhi yao beki Hassan Kessy na mshambuliaji Ibrahim Ajib.
Akizungumza katika Mkutano na Waandishi wa Habari Jumanne katika Hoteli ya Collessium, Barabara ya Nyerere, Dar es Salaam, Aveva alisema wachezaji hao walifanya vitendo ambavyo vimewaondolea uaminifu katika klabu.
Aveva alisema Kessy alitolewa kwa kadi nyekundu katika mchezo wa Ligi Kuu na baada ya adhabu hiyo, klabu ikaamua kumuongezea adhabu, lakini kabla hajamaliza adhabu zake akaibuka kusaini kwa mahasimu Yanga
Kuhusu Ajib, Aveva alisema mshambuliaji huyo alitolewa kwa kadi nyekundu katika mchezo wa Ligi Kuu pia na asubuhi yake akapanda ndege kwenda Afrika Kusini.
Amesema mambo kama hayo pamoja na uendeshwaji mbovu wa Ligi Kuu unaofanywa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) vimechangia Simba SC kufanya vibaya msimu huu. 
Aveva amesema kutakuwa na Mkutano Mkuu wa klabu Julai 10, mwaka huu kujadili matatizo ya klabu na kutafuta suluhisho lake.
Kauli ya Aveva inakuja baada ya Ibrahim Ajib kufuzu majaribio katika klabu ya Lamontville Golden Arrows FC ya Ligi Kuu ya ABSA Afrika Kusini.
Hata hivyo, klabu hiyo haiko tayari kumnunua mchezaji huyo bali inataka kumchukua kama mchezaji huru na kumsainisha mkataba.
Kwa sababu hiyo, klabu hiyo imemtaka Ajib kurejea klabuni mwake kuangalia kama Mkataba wake umekwisha apeleke uthibitisho Afrika Kusini ili apewe Mkataba Arrows.
Wakala wa mchezaji huyo, Juma Ndabila ameliambia Lete Raha kwamba wanarejea Dar pamoja na Ibrahim Ajib.
 “Amefuzu majaribio, lakini kuna suala la mkataba hapa, yeye alisema kamaliza mkataba, na Simba wanasema bado ana mkataba, kwa hivyo anarudi kutatua hilo suala,” amesema Ndabila.
Kwa upande wake, wakala aliyemuunganishia majaribio Ajib Afrika Kusini, Rodgers Mathaba amesema kwamba mchezaji huyo amepewa fursa ya kurudi Arrow wakati wowote akiwa mchezaji huru.
“Amefuzu majaribio, sasa ni juu yake anatakiwa hapa kama mchezaji huru, anarudi Dar es Salaam kushughulikia mkataba wake, nafasi yake ipo wazi hapa wakati wowote,” amesema Mathaba.