Monday, 8 August 2016

"NINA UHAKIKA NA UBINGWA MSIMU UJAO"- GEOFREY NYANGE 'KABURU'

Makamu mwenyekiti wa klabu ya Simba, amewaambia mashabiki wa timu hiyo kujiandaa na Ubingwa wa ligi ya Vodacom msimu ujao.
Kaburu ameiambia Goal kwamba mabadiliko ya kikosi walichosajili kwa ajili ya msimu ujao ndivyo vinavyo wapa matumaini ya kubeba taji hilo msimu ujao.
"Mabadiliko yetu hayapo kwenye uongozi bali hata usajili wetu wa msimu ujao umetulia tumesajili vizuri na ninauhakika na ubingwa msimu ujao" amesema kaburu.
Simba ambayo msimu ujao itakuwa chini ya kocha Mcameroon Joseph Omog jana ilikamilisha usajili wake wa msimu ujao akiwemo mchezaji Lodit Mavugo aliyetokea Vital'o ya Burundi.

No comments:

Post a Comment