KLABU
ya soka ya Simba haikuweza kufanya vizuri msimu uliopita katika Ligi Kuu ya
Tanzania Bara, kwani kutoka bingwa mtetezi iliambulia nafasi ya tatu msimu
uliopita na kuiacha Yanga ikitwaa ubingwa.
Hadi
kutwaa nafasi ya tatu, Simba ilipambana vilivyo kwani Kagera Sugar nayo ilikuwa
ikiwania nafasi hiyo kwa udi na uvumba. Jitihada za wachezaji na benchi la
ufundi ndizo zilizoifanya Simba kutwaa nafasi ya tatu.
Usajili
ukiwa unaendelea, Simba imeshamsajili kipa Andrew Ntala kutoka Kagera Sugar,
huku tayari ikiwa na makipa Juma Kaseja na Abel Dhaira. Usisahau yule wa kikosi
cha pili cha timu hiyo.
Wakati
Simba ikilundika makipa hao, mkongwe Kaseja ni kama hatakiwi tena na timu hiyo,
kwani kitendo cha kumsajili kipa namba moja wa Kagera, Ntala huku Dhaira
akiwepo kikosini inaonyesha wazi mmoja kati ya Kaseja au Dhaira anatakiwa
kuondoka.
Dhaira
hadi anatua Simba alikuwa kipa wa kutegemewa wa timu ya taifa ya Uganda, The
Cranes, hata huyu Ntala naye ni tegemeo la Kagera. Hii ina maana wote hao sasa
wanatakiwa kupambana na Kaseja kuwania nafasi ya kwanza kikosini.
Ni
ngumu kwa Simba kuachana na Dhaira kwani mkataba wake ni mkubwa na ambao
unaweza kuigharimu Simba kiasi kikubwa cha fedha kuuvunja.
Popote
pale duniani, huwezi kusajili makipa namba moja wawili kutoka timu nyingine huku
tayari ukiwa na kipa hodari. Hii ni sawa na usajili mwingine wa nafasi nyingine
uwanjani.
Tayari
kuna tetesi kwamba, Simba ipo tayari kumwachia Kaseja ajiunge na klabu nyingine
kwa madai ya kushuka kiwango na kushindwa kuisaidia timu kushika moja kati ya
nafasi mbili za juu.
Mchakato
mzima wa kuhakikisha Kaseja anaondoka Simba unaongozwa na kiongozi mmoja ambaye
sasa ana sauti ndani ya klabu hiyo na mbaya zaidi hakuna sababu za msingi za
kumuacha Kaseja.
KUSHINDWA
KUISAIDIA SIMBA
Sababu
kwamba Kaseja ameshindwa kuisaidia Simba haingii akilini kutokana na ukweli
kwamba hata katika mechi ambazo Simba imefungwa Kaseja akiwa langoni, kuna vitu
vingi vilikuwa vinatokea.
Hadi
sasa hakuna hoja ya msingi iliyotolewa na uongozi juu ya mpango huo
unaotengenezwa wa kuhakikisha Kaseja anaondoka Simba kwa njia yoyote ile, bali
inayolazimishwa ni hii ya kushindwa kuisaidia timu.
Hawafafanui
jinsi kipa huyu alivyoshindwa kuisaidia Simba kushika moja kati ya nafasi mbili
za juu, kwani hajawahi kufungwa mabao manne katika mechi moja na idadi kubwa ya
kufungwa kwake katika mchezo mmoja haizidi mabao matatu.
No comments:
Post a Comment