Monday, 8 August 2016

"NINA UHAKIKA NA UBINGWA MSIMU UJAO"- GEOFREY NYANGE 'KABURU'

Makamu mwenyekiti wa klabu ya Simba, amewaambia mashabiki wa timu hiyo kujiandaa na Ubingwa wa ligi ya Vodacom msimu ujao.
Kaburu ameiambia Goal kwamba mabadiliko ya kikosi walichosajili kwa ajili ya msimu ujao ndivyo vinavyo wapa matumaini ya kubeba taji hilo msimu ujao.
"Mabadiliko yetu hayapo kwenye uongozi bali hata usajili wetu wa msimu ujao umetulia tumesajili vizuri na ninauhakika na ubingwa msimu ujao" amesema kaburu.
Simba ambayo msimu ujao itakuwa chini ya kocha Mcameroon Joseph Omog jana ilikamilisha usajili wake wa msimu ujao akiwemo mchezaji Lodit Mavugo aliyetokea Vital'o ya Burundi.

JOSE MOURINHO: "HATIMAYE TUMEMPATA PAUL POGBA"

Meneja wa Manchester United, Jose Mourinho amekiri kuwa "hatimaye" klabu yake imefanikiwa kuipata huduma ya Paul Pogba kutoka Juventus
Mustakabali wa Pogba ulikuwa umezungukwa na tetesi nyingi mno majuma ya hivi karibuni, kwa nyota huyo kusajiliwa kwa ada ya kuvunja rekodi na Mashetani Wekundu.
Uthibitisho rasmi ulipatikana leo kutoka klabuni hapo kwamba Mfaransa huyo amepewa ruhusa na Juventus kuendelea na vipimo Manchester, lakini Mourinho ameonya kuwa hana uhakika wa namba katika kikosi chake.
"Pogba? Hatimaye, ni mchezaji mahiri. Mchezaji mzuri kama yeye atakuwa pamoja nasi, hatimaye tunaye," alisema Mourinho.
"Hatimaye tunaye. Anaungana na kikosi cha ushindi. Lakini atalazimika kufanya bidii nyingi kuingia kwenye kikosi. United ni klabu sahihi ambayo itamweka kwenye viwango anavyohitaji kuwa.
"Nimemwona Pogba akikimbia, akicheza kikapu, hufanya kila kitu, kwahiyo natumai atakuwa fiti. Nitakuwa nikimsubiri Jumanne."
Mourinho amenyanyua taji lake la kwanza kama meneja wa United kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Leicester City katika mechi ya Ngao ya Jamii iliyopigwa Wembley Jumapili mchana.

Oscar Pistorius ajeruhiwa gerezani

Msemaji wa idara ya magereza nchini humo, amesema kuwa Pistorius alianguka kutoka juu ya kitanda chake, lakini kwa sasa amerejeshwa gerezani anakohudumia kifungo cha miaka sita kwa kosa la kumuuwa mpenziwe wa kike Reeva Steenkamp.
Kuna ripoti inayosema kuwa alikuwa amejeruhiwa kwenye kifundo cha mkono.
Kumeibuku uvumi katika mitandao ya kijamii nchini Afrika Kusini kuwa Pistorius alikuwa amejaribu kujitia kitanzi lakini hilo limekanushwa na familia ya mwanariadha huyo.
Mwezi uliopita, waendesha mashtaka nchini Afrika Kusini, walisema kuwa watakata rufaa kupinga hukumu ya miaka sita ya Pistorius, wakisema kuwa ni hukumu ndogo mno.
Mwanariadha huyo alimuuwa mpenziwe wa kike , kwa kumpiga risasi nyumbani kwake wakati wa siku kuu ya wapendanao mnamo mwaka wa 2013, akisema kuwa alidhania ni mwizi.

Sakata la Yanga

Nafurahi kuona Tanzania inafufuka katika sokaa!!
Natamani kuona kila pedeshyeeee akimiliki timu moja ya ligi juu na kujenga kiwanja maendeleo ya timu yasonge mbele!!!
Yanga na sakata lao muwaaachie wenyewe ,majibu mtayapata baaada ya miaka 4 ,natumai wengine mtajifunza hapo

Pogback

Pogba ameshatua London na ameshafanyiwa vipimo Leo kutangazwa rasmiii!!

Saturday, 30 July 2016

Wauawa kwa kushindwa kulipa deni la biskuti India

Mtu mmoja na mkewe kutoka jamii ya Daliti inayobaguliwa tangu jadi nchini India wameuawa, mmoja akiwa amekatwa kichwa na mwengine kunyongwa kwa kushindwa kulipa deni la Rupee kumi na tano ambalo ni karibu senti ishirini na mbili tu.
Polisi kaskazini mwa taifa hilo wamethibitisha kisa hicho ambapo yasemekana mfanyi biashara anayetokea jamii ya hadhi ya juu,aliwaua wanandoa hao kwa kushindwa kulipa deni la biskuti walizokuwa wamewachukulia watoto wao.
Mfanyi biashara huyo amekamatwa.
Ubaguzi kwa misingi ya kijamii umeenea sana nchini India, huku watu wa jamii ya Daliti waliokuwa wamebadikwa jina la 'the untouchables' wakiwekwa kwenye daraja la chini kabisa kwenye sera hiyo ya kibaguzi nchini India iitwayo 'caste' ambapo wananyimwa fursa nyingi za kimaendeleo na hivyo kubaki katika lindi la umaskini .
Hata hivyo Visa vya ukatili wa kibaguzi dhidi ya jamii ya Dalit katika jimbo la Gujarat vimeongezeka mnamo siku za hivi karibuni na vimesababisha wimbi la maandamano kutoka watu wa jamii hiyo.

Thursday, 28 July 2016

Chelsea 1 Liverpool 0: Cahill´s header seals win

Gary Cahill's first-half header was enough for a 10-man Chelsea to see off Liverpool 1-0 in their International Champions Cup fixture.
Defender Cahill rose highest from a Cesc Fabregas corner in the 10th minute, heading it past Liverpool goalkeeper Loris Karius for the only goal of the game on Wednesday.
Jurgen Klopp's side could not find a way past Asmir Begovic despite Fabregas being sent off for a crunching tackle on Ragnar Klavan in the 70th minute at the Rose Bowl in Pasadena, California.
The loss was Liverpool's first of the pre-season under Klopp, having secured victories over Tranmere Rovers, Fleetwood Town, Wigan Athletic and Huddersfield Town.
Here's @GaryJCahill celebrating his goal earlier on... #CFCTour pic.twitter.com/daAhxVsMhu
— Chelsea FC (@ChelseaFC) July 28, 2016
Youngster Ovie Ejaria looked bright for the Reds, but it was Chelsea who were carving the better of the chances throughout the opening period, with Fabregas and Victor Moses particularly threatening.
Liverpool recruit Marko Grujic was in the wars in the first period and had to be treated on the stroke of half-time after a clash of heads, and was replaced at the break by Adam Lallana.
Chelsea sat back in the second half as head coach Antonio Conte tinkered with his side, with Juan Cuadrado, Pedro and new signing Michy Batshuayi entering the fray.
However, just three minutes later Conte's side were dealt a blow after Fabregas was given his marching orders for a studs-up challenge on Estonian defender Klavan.